Leucho wa Brindisi

Mchoro wa Oronzo Tiso, Mahubiri ya Leucho, Kanisa kuu la Brindisi.

Leucho wa Brindisi, mzaliwa wa Aleksandria, alikuwa askofu wa kwanza wa mji huo wa Italia Kusini katika karne ya 4.

Kabla ya hapo alikuwa mmonaki katika nchi yake, Misri.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 11 Januari[1].

  1. Martyrologium Romanum

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne