Lome

Jiji la Lome
Nchi Togo

Lomé ni mji mkuu wa Togo katika Afrika ya Magharibi pia mji mkubwa wa nchi hiyo pamoja na kuwa kitovu chake cha kiutawala na kiuchumi ukiwa na wakazi wanaokadiriwa kuwa 796,000 (mwaka 2006). Iko mwambaoni mwa Ghuba ya Guinea ya Atlantiki kwenye pwani fupi ya Togo yenye upana wa km 52 pekee. Mji uko karibu na mpaka wa Ghana.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne