Lucky Dube | |
---|---|
Jina la kuzaliwa | Lucky Philip Dube |
Amezaliwa | Ermelo, Transvaal (now Mpumalanga), Afrika Kusini | Agosti 3, 1964
Amekufa | 18 Oktoba 2007 (umri 43) Rosettenville, Johannesburg Gauteng, South Africa |
Aina ya muziki | reggae, mbaqanga |
Kazi yake | Mwanamuziki |
Ala | Sauti, Kinanda |
Miaka ya kazi | 1982 - 2008 |
Studio | Rycodisc, Gallo Record Company |
Ame/Wameshirikiana na | The Love Brothers |
Tovuti | Official website |
Lucky Philip Dube (tamka doo-bei) [1] (3 Agosti 1964 - 18 Oktoba 2007) alikuwa mwanamuziki wa reggae kutoka Afrika Kusini. Alirekodi albamu 22 katika lugha ya Kizulu, Kiingereza na Kiafrikaans katika kipindi cha miaka 25 na alikuwa mwanamuziki wa Reggae kutoka Afrika Kusini ambaye aliuza albamu nyingi kabisa. [2] [3] Dube aliuawa katika kitongoji cha Rosettenville huko Johannesburg jioni ya 18 Oktoba, mwaka 2007. [3] [4] [5]