Lushoto (mji)

Lushoto
Lushoto is located in Tanzania
Lushoto
Lushoto

Mahali pa mji wa Lushoto katika Tanzania

Majiranukta: 4°46′48″S 38°16′48″E / 4.78000°S 38.28000°E / -4.78000; 38.28000
Nchi Tanzania
Mkoa Tanga
Wilaya Lushoto
Idadi ya wakazi
 - Wakazi kwa ujumla 21,870
Ramani ya Wilaya ya Lushoto, Tanzania
Kikundi cha mazoezi ya kukimbia, Lushoto,Tanzania

Lushoto ni mji mdogo uliopo kwa kimo cha mita 1930 juu ya UB kwenye milima ya Usambara na ni makao makuu ya wilaya ya Lushoto.

Kiutawala ni kata moja tu na kwa mujibu wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, kata ilikuwa na wakazi wapatao 28,190 waishio humo. Katika sensa ya mwaka 2022 wakazi walihesabiwa 21,870 [1].

Kuna barabara ya lami kati ya Lushoto na Mombo inapounganika na barabara kuu B1 Arusha - Dar es Salaam.

Mazingira ya Lushoto yanafaa kwa kilimo; pia kuna vivutio vya utalii.

  1. https://www.nbs.go.tz

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne