Mainchin

Mainchin (kwa Kieire: Mainchín mac Setnai; alifariki Limerick, Ireland, mwishoni mwa karne ya 6 au mwanzoni mwa karne ya 7) anasemekana kuwa askofu wa mji huo. Jina lake linamaanisha "Mmonaki mdogo"; aliitwa pia "Mwenye hekima"[1].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 2 Januari[2].

  1. http://www.santiebeati.it/dettaglio/36135
  2. Martyrologium Romanum

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne