Kitabu cha Mambo ya Nyakati katika Tanakh (yaani Biblia ya Kiebrania) kimegawanywa sehemu mbili katika Biblia ya Kikristo na kupangwa katika ya vitabu vya historia.
Sehemu ya pili kinaitwa Kitabu cha pili cha Mambo ya Nyakati kikianzia na habari za mfalme Solomoni.
Kama vitabu vingine vyote vya Biblia, hiki pia kinatakiwa kisomwe katika mfululizo wa historia ya wokovu ili kukielewa kadiri ya maendeleo ya ufunuo wa Mungu kwa binadamu.