Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (pia huitwa kwa Kiingereza: Tanzania Communications Regulatory Authority ambapo mara nyingi huitwa kwa kifupi: TCRA) ni taasisi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yenye majukumu ya kusimamia sekta za mawasiliano na utangazaji.[1]

TCRA Ilianzishwa kwa Sheria ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania Na. 12 ya mwaka 2003 kusimamia huduma za kielektroniki na posta na masafa ya mawasiliano nchini Tanzania. Mamlaka ilianza kazi tarehe 1 Novemba 2003 na inafanya shughuli za zilizokuwa Tume ya Mawasiliano Tanzania (TCC) na Tume ya Utangazaji Tanzania (TBC).

  1. "Tanzania Communications Regulatory Authority". Commonwealth of Nations (kwa American English). Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2022-06-07. Iliwekwa mnamo 2022-06-30.

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne