Mapinduzi

Mashambulizi ya Bastille, 14 Julai 1789 ndiyo mwanzo wa Mapinduzi ya Ufaransa, ambayo ndiyo maarufu kuliko yote.
George Washington, kiongozi wa Mapinduzi ya Marekani (1775-1783).
Sun Yat-sen, kiongozi wa Xinhai Revolution huko China mwaka 1911.
Vladimir Lenin, kiongozi wa Mapinduzi ya Urusi ya mwaka 1917.

Mapinduzi (kutoka kitenzi "kupindua" juu chini) ni mabadiliko ya haraka upande wa siasa na miundo yanayotokana na shinikizo la wananchi, linalotumia mara nyingi nguvu.

Katika historia ya binadamu mapinduzi yalitokea mara nyingi kwa sababu, mbinu, muda na malengo mbalimbali.

Hayo yalifuatwa na athari kubwa juu ya utamaduni na uchumi wa jamii husika.

Pengine mabadiliko hayo ya mwisho pia yanaitwa mapinduzi hata yasiposababisha serikali ianguke.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne