Kwa matumizi mengine ya jina angalia maporomoko
Maporomoko ya maji ni mahali ambako maji yanatelemka juu ya kona kwenye mtelemko na kuelekea chini. Kwa kawaida ni sehemu ya njia ya mto au kijito pale ambako maji yanatelemka juu ya ukingo wa mwamba. Lakini inaweza kutokea pia kwenye ukingo wa barafuto pale ambako maji ya myeyuko yanatelemka.