Marathoni ya Frankfurt ni mbio ya Marathoni inayofanyika kila mwaka huko Frankfurt/Main nchini Ujerumani tangu kuanzishwa kwake 1981. Nchini Ujerumani ni mbio ndefu zaidi inayofanyika ndani ya mji fulani na mbio kubwa ya pili kwa idadi ya wakimbiaji wanaomaliza mbio yote. Jina rasmi lilikuwa "Commerzbank Frankfurt Marathon" na tangu mwaka 2011: "BMW Frankfurt Marathon".