Maria Magdalena Postel

Sanamu ya Marie-Madeleine Postel, Basilika la Utatu, Cherbourg.

Maria Magdalena Postel, ambaye jina la kiraia kwa Kifaransa lilikuwa Julie Françoise-Catherine Postel (Barfleur, Ufaransa, 28 Novemba 1756 - Saint-Sauveur-le-Vicomte, 16 Julai 1846) alikuwa mwanamke ambaye mwaka 1807 alianzisha shirika la Masista wa Shule za Kikristo wa Huruma (Congrégation des sœurs des Écoles chrétiennes de la Miséricorde) kwa ajili ya malezi ya Kikristo ya wasichana fukara [1].

Alitangazwa na Papa Pius X kuwa mwenye heri mwaka 1908 akatangazwa na Papa Pius XI kuwa mtakatifu tarehe 24 Mei 1925.

Sikukuu yake inaadhimishwa siku ya kifo chake, 16 Julai[2].

  1. https://www.santiebeati.it/dettaglio/91039
  2. Martyrologium Romanum

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne