Marinus na Asteri

Marinus na Asteri (walifariki Kaisarea Baharini, leo nchini Israeli, 262) walikuwa Wakristo ambao walikatwa kichwa kwa sababu ya imani yao chini ya Kaizari Galienus ingawa yeye alikuwa amesimamishwa dhuluma[1] [2].

Marinus alikuwa akida ambaye aliposhtakiwa na askari mwenzake akaungama wazi imani yake mbele ya hakimu akakatwa kichwa [3]. Basi, Asteri, seneta wa Dola la Roma, alitandaza joho lake chini kupokea maiti kwa heshima; kwa ajili hiyo yeye pia akakatwa kichwa hapohapo.

Tangu kale wanaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama watakatifu wafiadini.

Sikukuu yao huadhimishwa tarehe 3 Machi[4][5].

  1. "Martyr Marinus the Soldier at Caesarea in Palestine", Orthodox Church in America
  2. http://www.santiebeati.it/dettaglio/43750
  3. Eusebius Pamphilius, "The Martyrdom of Marinus at Caesaria", Church History, Chap. XV, CCEL
  4. Martyrologium Romanum
  5. Baronio S., Cesare (1631). Martyrologium Romanum (kwa latin). uk. 146.{{cite book}}: CS1 maint: unrecognized language (link)

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne