Mauzo dijitali (kwa Kiingereza "digital marketing") ni mbinu ya kutangaza biashara na kutafuta wateja inayoegemea matumizi ya mtandao. Huwa pia inahusu mauzo kwa kutumia simu za rununu, talakilishi au vifaa vingine vya kidijiti[1]
Ukuaji wake katika miaka ya 1990 na 2000 kwa sababu ya mapinduzi ya teknolojia ya intaneti ulibadilisha jinsi chapa na biashara zinavyotumia teknolojia kufanya mauzo. Mbinu za mauzo dijitali zimeenea kutokana na kuongezeka kwa wingi kwa watu wanaotumia vifaa vya kidijitali na kujumuishwa kwa majukwaa ya kidijitali katika mipango ya ununuzi na maisha ya kila siku [2] [3]. Mbinu za mauzo dijitali ni kama uimarishaji wa mashine za kutafuta tovuti (kwa Kiingereza "search engine optimization"), mauzo mashine za kutafuta tovuti (kwa Kiingereza "search engine marketing"), mauzo maudhui, mauzo waraghbishi, mauzo yanayoendeshwa na data, mauzo ya mitandao ya kijamii, uboreshaji wa mitandao ya kijamii na mauzo barua pepe. Njia nyingine ni pamoja na kutumia mbinu ya mauzo shirikishi. [4]
{{cite web}}
: More than one of |accessdate=
na |access-date=
specified (help)CS1 maint: date auto-translated (link)
{{cite web}}
: CS1 maint: date auto-translated (link)
{{cite web}}
: CS1 maint: date auto-translated (link)