Mazinguo

Yesu akipunga pepo bubu kadiri ya Gustav Doré, 1865.

Mazinguo (kutoka kitenzi kuzingua, kinyume cha kuzinga; pia: kupunga; kwa Kiingereza: exorcism kutoka Kigiriki: ἐξορκισμός, uapisho) ni dua za kuondoa pepo au viumbe wa kiroho wanaofikiriwa kuleta madhara kwa binadamu au mazingira yake[1].

Vitendo vya namna hiyo vinafanyika toka kale katika dini mbalimbali.

Mtu anayetoa huduma hiyo anaitwa mzinguaji. Katika historia baadhi ya watu wa namna hiyo walipata kuwa maarufu sana, kama vile Yesu.

  1. Jacobs, Louis (1999). "Exorcism". A Concise Companion to the Jewish Religion. doi:10.1093/acref/9780192800886.001.0001. ISBN 9780192800886.

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne