Mbinga (mji)

Mbinga ni mji katika Mkoa wa Ruvuma nchini Tanzania iliyopata kuwa halmashauri ya pekee mwaka 2015.

Mji huo ulikuwa na kata 20 na wakazi wake walikadiriwa kuwa 140,747 mnamo 2015[1]. Katika sensa ya mwaka 2022 walihesabiwa 158,896 [2].

Mbinga inapitiwa na barabara ya A19 kutoka Songea kwenda Mbamba Bay kwenye mwambao wa Ziwa Nyasa.

Wenyeji wa Mbinga ni Wamatengo.

  1. Makadirio ya Idadi ya Watu katika Majimbo ya Uchaguzi kwa Mwaka 2016,Tanzania Bara, tovuti ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Wizara ya Fedha na Mipango
  2. https://www.nbs.go.tz

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne