Mgagani

Mgagani
Migagani
Migagani
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Plantae (Mimea)
(bila tabaka): Angiospermae (Mimea inayotoa maua)
(bila tabaka): Eudicots (Mimea ambayo mche wao una majani mawili)
(bila tabaka): Rosids (Mimea kama mwaridi)
Oda: Brassicales (Mimea kama kabichi)
Familia: Cleomaceae (Mimea iliyo na mnasaba na mgagani)
Jenasi: Cleome (Migagani)
L.
Spishi: C. gynandra
(L.) Briq.

Migagani, migange, mikabili au miangani ni mimea ya jenasi Cleome katika familia na oda Brassicales (kabichi). Mgagani wa kawaida, Cleome gynandra, huliwa takriban kila mahali pa Afrika na katika mabara mengine pia. Wanawake wengi wenye mimba au waliozaa hula mmea huu, kwa sababu una chuma nyingi kiasi na husaidia kuongeza damu[1]. Mboga ya mgagani huitwa magagani.

  1. https://www.researchgate.net/publication/284809602_Nutritional_and_medicinal_properties_of_Cleome_gynandra

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne