Mmomonyoko

Bonde la mto wa Colorado/Marekani (Grand Canyon) ni tokeo la mmomonyoko wa maji

Mmomonyoko (kwa Kiingereza erosion) ni hali ya kuvunjika au kumegekamegeka kwa udongo au mwamba kutokana na athira ya upepo, maji, barafu, joto au mwendo wa ardhi. Kazi za binadamu zimekuwa pia sababu muhimu ya mmomonyoko.

Katika mazingira yanayokaliwa na binadamu, na hasa kwa kilimo, mmomonyoko unaleta hatari.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne