Mmomonyoko (kwa Kiingereza erosion) ni hali ya kuvunjika au kumegekamegeka kwa udongo au mwamba kutokana na athira ya upepo, maji, barafu, joto au mwendo wa ardhi. Kazi za binadamu zimekuwa pia sababu muhimu ya mmomonyoko.
Katika mazingira yanayokaliwa na binadamu, na hasa kwa kilimo, mmomonyoko unaleta hatari.