Mr. Blue

Mr. Blue
Mr. Blue kwenye pozi.
Mr. Blue kwenye pozi.
Maelezo ya awali
Jina la kuzaliwa Kheri Sameer Rajabu
Amezaliwa 14 Aprili 1987 (1987-04-14) (umri 37)
Aina ya muziki R&B na Bongo Flava
Kazi yake Mwimbaji
Ala Sauti
Miaka ya kazi 1999-
Studio G. Records, Dhahabu Records, 41 Records
Ame/Wameshirikiana na TID
Lady Jay Dee, K-Lyin

Khery Sameer Rajab (anafahamika zaidi kwa jina lake la kisanii kama Mr. Blue; amezaliwa 14 Aprili 1987) ni msanii wa muziki wa R&B na Bongo Flava kutoka nchini Tanzania.

Alifanikiwa kujizolea umaarufu mkubwa huku akipendwa na wapenzi na mashabiki wa muziki wake, mara tu baada ya kuingia katika fani ya muziki na wimbo wake 'Mr Blue'. Ambapo baadaye ikaja kuwa kama ndiyo jina lake la kisanii.

Mr Blue alikuwa gumzo kabla ya kuja kupata umaarufu zaidi na wimbo wake wa 'Mapozi', ambao ndiyo uliomzidishia kupendwa kutokana na mpangilio wa mashairi na sauti aliyotumia pamoja na maujanja ya ala ya muziki wenyewe.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne