Muziki wa Kigregori

Wimbo wa mwanzo Gaudeamus omnes, ulioandikwa kwa nota maalumu za mraba katika karne ya 14 au 15.


Muziki wa Kigregori ni aina nyofu ya muziki wa Kikristo inayotumia sauti moja tu tena bila ya kusindikizwa na ala yoyote.

Ndio muziki rasmi wa Kanisa la Kilatini[1] ambao ulistawi Ulaya magharibi na ya kati katika karne ya 9 na ya 10.

Jina linatokana na hadithi ya kwamba Papa Gregori I ndiye aliyeagiza utumike kanisani.

  1. The Constitution on the Sacred Liturgy, Second Vatican Council Archived 2012-12-20 at Archive.today; Pope Benedict XVI: Catholic World News 28 June 2006 both accessed 5 July 2006

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne