Mwandiko wa kikabari

Kutoka picha ya kichwa (1-3) kwa alama ya kikabari (4) iliyorahisishwa zaidi katika mwendo wa karne kumaanisha tu sauti ya "sag"
Maendeleo ya mwandiko wa kikabari
safu 1: picha asilia;
safu 2: mwandiko uliorahisishwa wakati wa Hammurabi;
safu 3: wakati wa Ashuri;
safu 4: wakati wa Babeli Mpya mnamo 600 KK;
safu 5: maelezo ya picha asilia na maana ya silabi iliyopatikana baadaye

Mwandiko wa kikabari ni kati ya aina za mwandiko wa kale sana duniani: ilikuwa kawaida katika Mesopotamia ya kale ukitumiwa na Wasumeri, Wababeli, Waashuri na wengine hata katika nchi jirani.

Ilianzishwa na Wasumeri mnamo mwaka 3,000 KK ikaishia baada ya mwaka 400 KK: mfano wa mwisho unaojulikana uliandikwa mwaka 75 BK.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne