Shirika la Mkataba wa Atlantiki ya Kaskazini (kwa Kiingereza: North Atlantic Treaty Organization, kifupi: NATO; kwa Kifaransa: Organisation du traité de l'Atlantique nord, kifupi: OTAN) ni ushirikiano wa kujihami wa kambi ya magharibi. Unaunganisha nchi 29 za Ulaya pamoja na Marekani na Kanada. Nchi wanachama zimeahidi kuteteana kama nchi moja inashambuliwa na nchi ya nje.
Makao makuu yapo Brussels.