NATO

Bendera ya NATO
Nchi wanachama wa NATO mnamo mwaka 2024 kwa rangi ya buluu.
Uenezi wa NATO hadi mwaka 2020.

Shirika la Mkataba wa Atlantiki ya Kaskazini (kwa Kiingereza: North Atlantic Treaty Organization, kifupi: NATO; kwa Kifaransa: Organisation du traité de l'Atlantique nord, kifupi: OTAN) ni ushirikiano wa kujihami wa kambi ya magharibi. Unaunganisha nchi 29 za Ulaya pamoja na Marekani na Kanada. Nchi wanachama zimeahidi kuteteana kama nchi moja inashambuliwa na nchi ya nje.

Makao makuu yapo Brussels.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne