Nazari na Chelsi

Nazari na Chelsi (waliosimama), mchoro wa Tiziano.

Nazari na Chelsi (walifariki labda Milano, Italia, 304 hivi) walikuwa Wakristo waliofia imani yao wakati wa dhuluma ya Dola la Roma.

Ambrosi aligundua masalia yao mwaka 395[1], lakini habari nyingi juu yao hazina msingi katika historia[2][3].

Tangu kale wanaheshimiwa na Wakatoliki, Waorthodoksi na wengineo kama watakatifu wafiadini.

Sikukuu yao huadhimishwa tarehe 28 Julai[4].

  1. Catholic Encyclopedia (1913), "Sts. Nazarius and Celsus" Retrieved 2012-03-04.
  2. http://www.santiebeati.it/dettaglio/64650
  3. Saint Gregory (Bishop of Tours) (1988). Raymond Van Dam, tr. (mhr.). Glory of the Martyrs. Liverpool: Liverpool University Press. ku. 69–70. ISBN 978-0-85323-236-0.
  4. Martyrologium Romanum

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne