Pakomi (Thebe, Luxor, 292 - Pbow 9 Mei 348) alikuwa askari, halafu mmonaki wa Misri, maarufu kwa kuanzisha abasia ya kwanza (320 hivi) na kwa kutunga kanuni ya kwanza ya maisha ya utawa.
Mpaka leo maisha hayo yanafuatwa hasa Ethiopia, lakini athari zake zinaonekana katika umonaki na mashirika mbalimbali ya kitawa, hata katika Kanisa la magharibi.
Anaheshimiwa na Kanisa Katoliki na madhehebu mengine mbalimbali ya Ukristo kama mtakatifu.
Sikukuu yake inaadhimishwa kila mwaka tarehe ya kufa kwake[1] au tarehe 15 Mei.