Papa Miltiades

Papa Miltiades.

Papa Miltiades alikuwa Papa kuanzia tarehe 2 Julai 311 hadi kifo chake tarehe 10 Januari 314[1]. Kadiri ya Liber Pontificalis, Miltiades alikuwa na asili ya Afrika[2], ingawa aliweza pia kuwa mtu wa Roma.[3]

Alimfuata Papa Eusebius akafuatwa na Papa Silvester I. Alifurahia amani ambayo Kanisa lilirudishiwa na kaisari Konstantino Mkuu, na ingawa alipingwa sana na Wadonati, alishughulikia kwa busara upatanisho[4].

Wakati wa Upapa wake Hati ya Milano iliwapa wananchi uhuru wa dini (313) na Kanisa lilirudishiwa mali yake iliyotaifishwa.

Alipinga fundisho la Donatus wa Carthago la kwamba mapadri na maaskofu walioasi wabatizwe tena. Uaumuzi huo wa Sinodi ya Laterano (313) haukumaliza uenezi wa farakano la Donato katika Afrika Kaskazini.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake[5].

  1. https://www.vatican.va/content/vatican/en/holy-father.index.html#holy-father
  2. https://dacb.org/stories/tunisia/militiades/
  3. Richard P. McBrien, Lives of the Popes, (HarperCollins, 2000), 56.
  4. Martyrologium Romanum
  5. Martyrologium Romanum: ex Decreto Sacrosancti oecumenici Concilii Vaticani II instauratum auctoritate Ioannis Pauli P.P. II promulgatum, Romae 2001, ISBN 8820972107

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne