Papa Paulo II (23 Februari 1417 – 26 Julai 1471) alikuwa Papa wa Kanisa Katoliki na mtawala wa Dola la Papa kuanzia tarehe 30 Agosti/16 Septemba 1464 hadi kifo chake[1]. Alitokea Venezia, Italia[2].
Jina lake la kuzaliwa lilikuwa Pietro Barbo.
Alimfuata Papa Pius II akafuatwa na Papa Sixtus IV.
Alipoona mjomba wake, Papa Eugenio IV, akichaguliwa, aliacha mafunzo ya biashara na kuingia katika masomo ya dini. Kupanda kwake madarakani ndani ya Kanisa kulikuwa kwa haraka, na alipochaguliwa kuwa Papa mwaka 1464, alikusanya kwa wingi sanaa na vitu vya kale. [3]