Papa Paulo VI (26 Septemba 1897 – 6 Agosti 1978) alikuwa Papa kuanzia tarehe 21/30 Juni 1963 hadi kifo chake[1]. Alitokea Concesio, Brescia, Italia[2].
Jina lake la kuzaliwa lilikuwa Giovanni Battista Enrico Antonio Maria Montini.
Alimfuata Papa Yohane XXIII akafuatwa na Papa Yohane Paulo I.
Alitangazwa na Papa Fransisko kuwa mwenye heri tarehe 19 Oktoba 2014 na mtakatifu tarehe 14 Oktoba 2018.