Papa Pius X (Riese, Veneto, Italia Kaskazini, 2 Juni 1835 – Roma, 20 Agosti 1914) alikuwa Papa kuanzia tarehe 4/9 Agosti 1903 hadi kifo chake[1]. Alitokea Riese, Treviso, Italia[2].
Jina lake la kuzaliwa lilikuwa Giuseppe Sarto.
Alimfuata Papa Leo XIII na kuvishwa taji la Kipapa tarehe 9 Agosti 1903, wa kwanza katika karne ya 20. Akafuatwa na Papa Benedikto XV.
Alitangazwa na Papa Pius XII kuwa mwenyeheri tarehe 3 Juni 1951, halafu mtakatifu tarehe 29 Mei 1954.