Popo

Popo
Popo-masikio wa Townsend (Corynorhinus townsendii)
Popo-masikio wa Townsend
(Corynorhinus townsendii)
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Mammalia (Wanyama wenye viwele wanaonyonyesha wadogo wao)
Ngeli ya chini: Eutheria
Oda: Chiroptera (Wanyama kama popo)
Ngazi za chini

Nusuoda 2:

Popo ni mamalia kama panya wenye mabawa.

Spishi zake nyingi sana hula wadudu: hizi zimo katika nusuoda Yangochiroptera.

Spishi kubwa za nusuoda hii hula ndege, mijusi, vyura na hata samaki.

Spishi chache za popo wanyonya-damu huko Amerika ya Kusini hula damu ya mamalia au ndege.

Familia Pteropodidae ya nusuoda Yinpterochiroptera ina spishi kubwa hadi ukubwa wa paka na uzito wa kilogramu moja; urefu wa mabawa pamoja unaweza kufikia sentimita 150. Spishi hizi hula matunda.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne