Preieto na Amarino

Sanamu ya Mt. Preieto.

Preieto na Amarino (walifariki Volvic, 25 Januari 676) walikuwa mmoja askofu wa 25 wa Alvernia, leo Clermont-Ferrand, nchini Ufaransa, na mwingine abati au mlei ambao waliuawa pamoja na matajiri wa mji huo[1][2].

Tangu zamani wanaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama watakatifu wafiadini[3].

Sikukuu yao inaadhimishwa kila mwaka tarehe 25 Januari[4].

  1. Henry Hart Milman, History of Latin Christianity (T.Y. Crowell, 1881), 398.
  2. Barbara H. Rosenwein, Emotional Communities in the Early Middle Ages (New York: Cornell University Press, 2006), 170.
  3. http://www.santiebeati.it/dettaglio/92179
  4. Martyrologium Romanum

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne