Puto ni chombo cha usafiri angani inatumia nguvu elezi ya gesi nyepesi kwa kubeba abiria na mizigo juu hewani. Inatembea kwa kusukumwa na upepo na njia ya pekee ya kuiongoza ni kuipandisha au kushusha. Ni tofauti na ndegeputo (purutangi) yenye injini inayoweza kulengwa na rubani yake.