Jiji la Pyongyang | |
Nchi | Korea Kaskazini |
---|
Pyongyang (kwa Kikorea: 평양 직할시 'Phyŏngyang chighalshi' kwa mwandiko wa Kilatini) ni mji mkuu, pia mji mkubwa wa Korea Kaskazini wenye wakazi 2,926,443 na pamoja na rundiko la mji watu 3,702,757 (2005). Ni kati ya mahali pachache ambako wageni wa nje wanaruhusiwa kutembelea.
Mji uko kusini-magharibi mwa nchi, karibu na mpaka na Korea ya Kusini. Pyongyang ni kitovu cha nchi kisiasa, kiutamaduni na kiuchumi.