Raffaello Sanzio (kwa Kiitalia huitwa pia Raffaello da Urbino; kwa Kiingereza anajulikana kama Raffael au Raphael) (6 Aprili 1483 - 6 Aprili 1520) alikuwa mchoraji na mjenzi kutoka Italia.
Pamoja na Leonardo da Vinci na Michelangelo huhesabiwa kati ya wasanii muhimu wa zama ya mwamko ya Italia.