Richadi wa Andria

Sanamu ya Mt. Richadi huko Andria.

Richadi wa Andria (Uingereza, karne ya 12 - Andria, Puglia, Italia, 1196 hivi) alikuwa askofu wa Andria kwa zaidi ya miaka 40[1][2].

Alipata umaarufu kwa maadili yake, miujiza mingi, pamoja na juhudi kubwa kwa ajili ya uinjilishaji mpya wa waumini.

Alishiriki mtaguso wa tatu wa Laterano (1179).

Alipokea pia kwa heshima masalia ya wafiadini Erasmo na Ponsyano[3].

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu, hasa baada ya kutangazwa rasmi na Papa Bonifasi VIII au Papa Eugeni IV[4].

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 9 Juni[5].

  1. St. Richard of Andria Catholic Online
  2. Saint Richard of Andria Patron Saint Index
  3. http://www.santiebeati.it/dettaglio/90917
  4. Storia della citta di Andria dalla sua origine sino al corrente anno 1841, by Riccardo D'Urso, page 102-104.
  5. Martyrologium Romanum

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne