Kundinyota | Kantarusi (Centaurus) |
Mwangaza unaonekana | +1.33 |
Kundi la spektra | G2 V |
Paralaksi (mas) | 754.81 ± 4.11 |
Umbali (miakanuru) | 4.37 |
Mwangaza halisi | 5.71 |
Masi M☉ | 1.1 |
Nusukipenyo R☉ | 1.22 |
Mng’aro L☉ | 1.5 |
Jotoridi usoni wa nyota (K) | 5790 |
Muda wa mzunguko | siku 41 |
Majina mbadala | α Centauri, Toliman, Bungula, Gliese 559, FK5 538, CD−60°5483, CCDM J14396-6050, GC 19728 |
Rijili Kantori , Rijili Kantarusi au ing. Alpha Centauri (pia: Toliman au Rigil Kentaurus) ni nyota inayong'aa sana katika anga ya kusini kwenye kundinyota la Kantarusi (pia: ing. Centaurus). Ni nyota angavu ya nne angani lakini haionekani kwenye nusu ya kaskazini ya Dunia.
Alpha Centauri ni nyota ya pekee kwa sababu ni nyota yetu jirani katika anga ina umbali wa miakanuru 4.2. Inaonekana angani karibu na kundinyota la Salibu (Crux).