Rijili Kantori

Rijili Kantori (Alfa Centauri, Rigil Kentaurus)
Rijili Kantori - Alpha Centauri katika kundinyota la Kantarusi
Kundinyota Kantarusi (Centaurus)
Mwangaza unaonekana +1.33
Kundi la spektra G2 V
Paralaksi (mas) 754.81 ± 4.11
Umbali (miakanuru) 4.37
Mwangaza halisi 5.71
Masi M☉ 1.1
Nusukipenyo R☉ 1.22
Mng’aro L☉ 1.5
Jotoridi usoni wa nyota (K) 5790
Muda wa mzunguko siku 41
Majina mbadala α Centauri, Toliman, Bungula, Gliese 559, FK5 538, CD−60°5483, CCDM J14396-6050, GC 19728


Rijili Kantori , Rijili Kantarusi au ing. Alpha Centauri (pia: Toliman au Rigil Kentaurus) ni nyota inayong'aa sana katika anga ya kusini kwenye kundinyota la Kantarusi (pia: ing. Centaurus). Ni nyota angavu ya nne angani lakini haionekani kwenye nusu ya kaskazini ya Dunia.

Alpha Centauri ni nyota ya pekee kwa sababu ni nyota yetu jirani katika anga ina umbali wa miakanuru 4.2. Inaonekana angani karibu na kundinyota la Salibu (Crux).


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne