Rizaburo Toyoda

Risaburo Toyoda (Machi 5, 1884Juni 3, 1952) alikuwa mfanyabiashara wa Kijapani na mkwe wa mwanzilishi wa Toyota Industries, Sakichi Toyoda. Pia alikuwa shemeji wa mwanzilishi wa Toyota Motor Corporation, Kiichiro Toyoda[1].

Awali, alikuwa na jina la ukoo Kodama. Alisoma katika Chuo Kikuu cha Kobe na Hitotsubashi. Mwaka 1939, aliteuliwa kuwa rais wa kwanza wa Toyota Motor Corporation. Alifariki akiwa na umri wa miaka 68.

  1. 豊田利三郎 とよだ りさぶろう デジタル版 日本人名大辞典+Plusの解説(Japanese)

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne