Ruvu (Pwani)

Kwa matumizi mengine ya jina hili angalia Ruvu (maana)

Ruvu (pwani)/Ruvu au Kingani
Ruvu (au Kingani) mnamo mwaka 1910 karibu na mdomo wake Bagamoyo
Chanzo Milima ya Uluguru, mitelemko ya mashariki
Mdomo Bahari Hindi, karibu na Bagamoyo
Nchi Tanzania
Urefu km 285
Tawimito upande wa kulia Mto Mgeta
Tawimito upande wa kushoto Mto Ngerengere
Eneo la beseni km² 17,700

Ruvu (zamani Kingani pia[1]) ni mto wa Mkoa wa Morogoro na Mkoa wa Pwani nchini Tanzania.

Unapokea hasa maji ya upande wa mashariki wa milima ya Uluguru na kuyapeleka Bahari Hindi.

Ruvu hii haina uhusiano na mto Jipe Ruvu wa mkoa wa Kilimanjaro / Upare.

  1. Linganisha makala "Kingani" katika Kamusi ya Koloni za Kijerumani: "Kingani oder Ruwu (d. i. Fluß)" - yaani Kingani au Ruvu (maanake mto)"

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne