Sabino wa Canosa

Mt. Sabino.

Sabino wa Canosa (Canosa di Puglia, Italia, 461 - Canosa di Puglia, 9 Februari, 566) alikuwa askofu wa mji huo kuanzia mwaka 514[1].

Rafiki wa Benedikto wa Nursia, alitumwa na Papa Agapeto I kwenda Konstantinopoli kutetea imani sahihi kuhusu utu halisi wa Yesu.

Tangu kale anaheshimiwa na Kanisa Katoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 9 Februari[2].

  1. http://www.santiebeati.it/dettaglio/40300
  2. Martyrologium Romanum

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne