Samweli

Mchoro mdogo unaomuonyesha Samweli akimweka wakfu mfalme Daudi.

Samweli (kwa Kiebrania: שְׁמוּאֵל Šəmuʼel, maana yake labda ni "Anayemsikiliza Mungu"; 1070 - 1000 KK hivi) ni mtu muhimu wa Historia ya wokovu ya Agano la Kale.

Katika Biblia anatajwa kama mwamuzi wa mwisho na mkuu kuliko wote, tena kama nabii tangu utotoni. Ndiye mwanzilishi wa ufalme wa Israeli kwa kuwa kwa agizo la Mungu alimpaka mafuta Sauli awe mfalme wa taifa lake, tena, baada ya huyo kukataliwa kwa ukaidi wake, alimpaka vilevile Daudi, ambaye kutoka uzao wake akaja kutokea Masiya[1].

Habari zake zinasimuliwa katika Vitabu vya Samweli.

Kanisa Katoliki na madhehebu mbalimbali za Ukristo vinamheshimu kama mtakatifu hasa tarehe 20 Agosti[2].

  1. https://www.santiebeati.it/dettaglio/66950
  2. Martyrologium Romanum

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne