Satelaiti (pia setelaiti, setilaiti, kutoka Kilatini satelles, "msindikizaji", kupitia Kiingereza satellite) ni kitu kinachofuatana na kitu kingine. Neno linatumiwa kwa maana mbili ambayo ni:
Kwa kufuata maana hii ya 2, Satelaiti au Setilaiti ni kifaa cha kuundwa na binadamu ambacho huundwa kwa kusudi la kukiweka kwenye obiti kwaajili ya shughuli maalumu kama vile utafiti wa kisayansi. Mara nyingine vifaa hivi huitwa satelaiti za kutengenezwa ili kuzitofautisha na satelaiti asilia kama vile mwezi wa Dunia.