Serafino wa Montegranaro

Mt. Serafino.

Serafino wa Montegranaro (154012 Oktoba 1604), alikuwa bradha wa shirika la Ndugu Wadogo Wakapuchini kutoka Italia ya Kati.

Fukara kweli, aling'aa kwa unyenyekevu na moyo wa ibada[1].

Mtawa huyo asiye na vipawa vingi kiutu, bali mwenye karama za ajabu, anaheshimiwa na Kanisa Katoliki kama mtakatifu tangu alipotangazwa na Papa Klementi XIII tarehe 16 Julai 1767.

Sikukuu yake inaadhimishwa kila mwaka tarehe 12 Oktoba[2].

  1. https://www.santiebeati.it/dettaglio/74050
  2. Martyrologium Romanum

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne