Sfinksi (kwa Kiingereza sphinx) ni kiumbe cha visasili katika tamaduni za Misri ya Kale, Ugiriki wa Kale na Mesopotamia. Inajulikana pia katika visasili na sanaa za Asia ya Kusini na Kusini-mashariki.
Inaunganisha mwili wa simba na kichwa cha binadamu.
Kisasili cha sfinksi za Mashariki ya Kati kwa kiasi kikubwa kimesahauliwa. Ni pekee kuhusu sfinksi ya Ugiriki ya kwamba hadithi kadhaa zimehifadhiwa.