Spaghetti

Spageti katika sufuria: maji ya chumvi yenye mafuta kidogo
Spageti alla Napoletana ni pamoja na mchuzi wa nyanya na jibini iliyosagwa juu yake
Spageti iliyoungwa kwa nyama na jibini.

Spageti (kwa Kiitalia: Spaghetti) ni chakula cha tambi chenye asili ya Italia Kusini. Ni tambi ya ngano yenye umbo jembamba kama kamba na urefu wa sentimeta 40.

Hupikwa katika maji kwa dakika chache na kuliwa kwa uma baada ya kuongeza michuzi mbalimbali.

Spageti ni aina mojawapo ya chakula cha pasta na neno linatumiwa wakati mwingine kutaja pasta kwa jumla.

Kutoka Italia chakula hicho kimeenea duniani kote kwa sababu hupikwa haraka, inaleta shibe nzuri na kuna njia nyingi za kubadilisha ladha yake.

Kwa njia ya utani zimekuwa ishara ya utamaduni wa Italia, jinsi inavyoonekana katika filamu za Spaghetti Western.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne