Swala pala | ||||||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
![]() Swala pala wa kawaida
(Aepyceros m. melampus) ![]() Swala pala uso-mweusi
(Aepyceros m. petersi) | ||||||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||||||
| ||||||||||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||||||||||
Nususpishi 2:
|
Swala pala au swalapala (Aepyceros melampus kutoka Kigiriki αιπος, aipos "juu" κερος, ceros "pembe" + melas "nyeusi" pous "mguu") ni swala ambaye si mkubwa sana kutoka Afrika. Jina Impala ambalo ni jina la swala pala kwa Kiingereza linatoka kutoka lugha ya Kizulu na linamaanisha "Swara". Wao hupatikana katika savana misitu nene nchini Kenya, Tanzania, Eswatini, Msumbiji, Namibia ya kaskazini, Botswana, Zambia, Zimbabwe, kusini mwa Angola, kaskazini mashariki mwa Afrika Kusini na Uganda. Swala pala wa kawaida wanaweza kupatikana katika idadi ya hadi 1,600,000 barani Afrika.[1]