Swala pala

Swala pala
Swala pala wa kawaida (Aepyceros m. melampus)
Swala pala wa kawaida
(Aepyceros m. melampus)
Swala pala uso-mweusi (Aepyceros m. petersi)
Swala pala uso-mweusi
(Aepyceros m. petersi)
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Mammalia (Wanyana wenye viwele wanaonyonyesha wadogo wao)
Oda: Artiodactyla (Wanyama wenye vidole viwili au vinne mguuni)
Nusuoda: Ruminantia (Wanyama wanaocheua)
Familia: Bovidae (Wanyama walio na mnasaba na ng'ombe)
J. E. Gray, 1821
Nusufamilia: Aepycerotinae (Swala pala)
J. E. Gray, 1872
Jenasi: Aepyceros
Sundevall, 1847
Spishi: A. melampus
Lichtenstein, 1812
Ngazi za chini

Nususpishi 2:

Swala pala au swalapala (Aepyceros melampus kutoka Kigiriki αιπος, aipos "juu" κερος, ceros "pembe" + melas "nyeusi" pous "mguu") ni swala ambaye si mkubwa sana kutoka Afrika. Jina Impala ambalo ni jina la swala pala kwa Kiingereza linatoka kutoka lugha ya Kizulu na linamaanisha "Swara". Wao hupatikana katika savana misitu nene nchini Kenya, Tanzania, Eswatini, Msumbiji, Namibia ya kaskazini, Botswana, Zambia, Zimbabwe, kusini mwa Angola, kaskazini mashariki mwa Afrika Kusini na Uganda. Swala pala wa kawaida wanaweza kupatikana katika idadi ya hadi 1,600,000 barani Afrika.[1]

  1. http://www.iucnredlist.org/apps/redlist/details/550/0/full

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne