Taarifa

Taarifa (kutoka neno la Kiarabu) ni habari maalumu inayowasilishwa ama kwa mdomo ama kwa maandishi.

Pia ni takwimu zilizochakatwa ambazo zina maana kamili inayoweza kutumika katika kufanya maamuzi fulani.

Mfano:

  • 1, 2, 3, 4, 5, 6... ni takwimu. Lakini
  • Orodha ya namba shufwa 2, 4, 6... ni taarifa.

Taarifa hutofautiana kulingana na muktadha kama ilivyo kwa takwimu.

Taarifa ya habari ni wasilisho la maelezo ya tukio au hali maalumu kwa jamii nzima linalopitia njia yoyote: redio, gazeti, runinga, mbiu au mikutano.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne