| |
Mahali | Afrika ya Mashariki |
Nchi zinazopakana | Burundi, Kongo, Tanzania, Zambia |
Eneo la maji | km² 32,893 kutegemeana na kiasi cha mvua |
Kina cha chini | kuanzia m 3.5 hadi 1,470 |
Mito inayoingia | Lufubu, Malagarasi, Ruzizi |
Mito inayotoka | Lukuga |
Kimo cha uso wa maji juu ya UB |
m 782 |
Miji mikubwa ufukoni | Bujumbura, Kalemie, Kigoma |
Ziwa Tanganyika ni moja ya maziwa makubwa ya Afrika ya Kati likienea mpakani mwa Tanzania, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Burundi na Zambia.
Ni ziwa kubwa la pili duniani kwa wingi wa maji matamu baada ya Ziwa Baikal (Siberia) kwa kuzingatia kiasi cha maji ndani yake na kina (hadi mita 1,470).
Kwa kulinganisha eneo lake (km² 32,893) ni la pili tu baada ya Viktoria Nyanza katika Afrika.
Maji yake hutoka kuelekea mto Kongo ha hatimaye katika Bahari Atlantiki.