Tanganyika (ziwa)

Ziwa Tanganyika
Ziwa Tanganyika jinsi linavyoonekana kutoka angani
Ziwa Tanganyika jinsi linavyoonekana kutoka angani
Mahali Afrika ya Mashariki
Nchi zinazopakana Burundi, Kongo,
Tanzania, Zambia
Eneo la maji km² 32,893 kutegemeana na kiasi cha mvua
Kina cha chini kuanzia m 3.5 hadi 1,470
Mito inayoingia Lufubu, Malagarasi, Ruzizi
Mito inayotoka Lukuga
Kimo cha uso wa maji
juu ya UB
m 782
Miji mikubwa ufukoni Bujumbura, Kalemie, Kigoma
Ziwa Tanganyika pamoja na miji muhimu kando lake

Ziwa Tanganyika ni moja ya maziwa makubwa ya Afrika ya Kati likienea mpakani mwa Tanzania, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Burundi na Zambia.

Ni ziwa kubwa la pili duniani kwa wingi wa maji matamu baada ya Ziwa Baikal (Siberia) kwa kuzingatia kiasi cha maji ndani yake na kina (hadi mita 1,470).

Kwa kulinganisha eneo lake (km² 32,893) ni la pili tu baada ya Viktoria Nyanza katika Afrika.

Maji yake hutoka kuelekea mto Kongo ha hatimaye katika Bahari Atlantiki.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne