Tungo

Utungo uliotokana na kutungwa kwa Shanga

Tungo ni neno au nomino inayotokana na kitenzi "tunga". Kutunga ni kuweka/kushikamanisha vitu pamoja kwa kutumia kitu kama kamba au uzi kwa kupitishia ndani yake. Kwa mfano, unaweza kutunga vitu kama samaki, shanga, simbi na kadhalika.

Unaposhikamanisha vitu pamoja tunapata kitu kinachoitwa utungo (mmoja) au tungo (nyingi).


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne