Tungo ni neno au nomino inayotokana na kitenzi "tunga". Kutunga ni kuweka/kushikamanisha vitu pamoja kwa kutumia kitu kama kamba au uzi kwa kupitishia ndani yake. Kwa mfano, unaweza kutunga vitu kama samaki, shanga, simbi na kadhalika.
Unaposhikamanisha vitu pamoja tunapata kitu kinachoitwa utungo (mmoja) au tungo (nyingi).