Tuzo ya Nobel

Alfred Nobel (1833 - 1896)
Medali ya Tuzo ya Nobeli
Medali ya Tuzo ya Nobeli
Ramani inayoonyesha idadi ya washindi wa Tuzo ya Nobel nchi kwa nchi
Wikimedia Commons ina media kuhusu:

Tuzo ya Nobel ni tuzo ya fedha kwa ajili ya mafanikio ya pekee katika fani mbalimbali. Ilianzishwa na Alfred Nobel.

Tangu mwaka wa 1901 imetolewa kwa watu waliofaulu katika fani zifuatazo: Fizikia, Kemia, Tiba (au Fiziolojia), Fasihi na Amani. Tangu mwaka wa 1969, tuzo ya sita imeongezwa kwa Uchumi. Siku hizi Tuzo ya Nobel ni tuzo ya kimataifa mashuhuri zaidi duniani. Wanaotuzwa hupokea hati, medali ya dhahabu na kiasi cha pesa cha takriban milioni 1,2 (kinategemea mapato ya riba yanayotokana na mfuko wa fedha iliyotengwa na Alfred Nobel kwa kusudi hili).

Maazimio kuhusu tuzo za kila mwaka hutolewa kufuatana na wasia wa Alfred Nobel na kamati zifuatazo:

  1. Tuzo ya Nobel ya Fizikia inateuliwa na Taasisi ya Taaluma ya Sayansi ya Sweden
  2. Tuzo ya Nobel ya Kemia inateuliwa na Taasisi ya Taaluma ya Sayansi ya Sweden
  3. Tuzo ya Nobel ya Tiba inateuliwa na Karolinska Institutet Stockholm
  4. Tuzo ya Nobel ya Fasihi inateuliwa na Taasisi ya Taaluma ya Sweden kwa lugha na fasihi
  5. Tuzo ya Nobel ya Amani inateuliwa na kamati ya Nobel ya Norway iliyochaguliwa na Bunge la Norway
  6. Tuzo ya Nobel ya Elimu ya Uchumi inateuliwa na Taasisi ya Taaluma ya Sayansi ya Sweden

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne