(makala hii inahusu kata ya Ubungo, kuangalia makala ya wilaya yake bonyeza hapa)
Kata ya Ubungo | |
Mahali pa Ubungo katika Tanzania |
|
Majiranukta: 6°47′42″S 39°15′58″E / 6.79500°S 39.26611°E | |
Nchi | Tanzania |
---|---|
Mkoa | Dar es Salaam |
Wilaya | Ubungo |
Ubungo ni kata ya wilaya ya Ubungo katika Mkoa wa Dar es Salaam, Tanzania, yenye postikodi namba 16103.
Ubungo ipo katika sehemu ya kati ya magharibi mwa wilaya na inafahamika sana Tanzania kama kitovu kikuu cha Mabasi yaelekeayo mikoani.
Kituo cha mabasi cha Ubungo kimeungana na baadhi ya vituo vikubwa vya miji mbalimbali ya Tanzania kama vile cha Arusha, Moshi, Morogoro, Dodoma, Mbeya, Iringa, Mtwara, Lindi, Singida, Tanga na Mwanza; vilevile hadi Nairobi, Lilongwe, Lusaka na miji mingine kadhaa ya Afrika ya Mashariki.
Pia Ubungo ndipo palipo makao makuu ya TANESCO, shirika la umeme la Tanzania.