Ufalme wa Ashanti

Ramani ya Ashanti.
Bendera ya Ashanti.

Ufalme wa Ashanti (pia Asante: Asanteman) ulikuwa milki ya Waashanti, ambao ni kundi mojawapo kati ya Waakan katika nchi ambayo ni Ghana ya kisasa. Ufalme wa Ashanti ulidumu kutoka mwaka 1701 hadi 1957 ukiendelea leo hii kama "mamlaka ya kimila" ndani ya Ghana. Mkuu wa milki ni mfalme mwenye cheo cha Asantehene. Mji mkuu ni Kumasi.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne