Ukuta wa Berlin

Ukuta wa Berlin mnamo mwaka 1980
upande wa kushoto: Berlin Mashariki (angalia kanda la mauti mbele ya ukuta wamapopita askari; hapo walinzi walipaswa kumfyatulia risasi kila mtu aliyeingia);
upande wa kulia: Berlin Magharibi ambako ukuta ulichorwa picha na vijana
Eneo la Berlin Magharibi lilikuwa kama kisiwa ndani ya Ujerumani Mashariki

Ukuta wa Berlin (kwa Kijerumani Berliner Mauer) ulitenganisha sehemu mbili za jiji la Berlin (Ujerumani) kuanzia 13 Agosti 1961 hadi 9 Novemba 1989. Ukuta huo ulikuwa na urefu wa kilomita 45.3 ukiwa sehemu ya mpaka kati ya madola mawili ya Ujerumani yaliyokuwepo kuanzia 1949 hadi 1990. Ukuta wa Berlin ulikuwa mfano uliojulikana zaidi wa "pazia la chuma" katika Ulaya lililotenganisha nchi za kikomunisti za Ulaya mashariki na nchi za Ulaya magharibi. Takriban watu 200 waliuawa walipojaribu kuvuka ukuta kutoka mashariki kwenda magharibi.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne